Simu mpya aina ya Smartphone zaingia Dar es Salaam

Zuri
Kampuni ya Zuri
ilio na makao yake mjini Hong Kong imezindua rasmi simu aina ya
Smartphone katika soko la Tanzania.Kampuni hiyo pia imeisajili kampuni
ya DESPEC kama msambazaji rasmi wa simu hizo nchini Kenya Tanzania na
Uganda.
''Tumeona kwamba kuna fursa nzuri ya bidhaa zetu Tanzania...tunawasihi raia wa Tanzania kujipatia simu zenye ubora ili kukwepa gharama zinazokuja na simu baada ya kununua mbali na maswala mengine ya kiafya yanahuhusishwa na simu zenye kiwango cha chini',afisa mkuu wa simu za Zuri Bwana Vikash Shah,amesema.
Kulingana na The Citizen Tanzania,Mkurungenzi wa kampuni ya DESPEC Bw Riyaz Jamal anaamini kwamba kwa kuongeza Zuri katika soko la simu kutawasaidia raia wa Tanzania kupata simu zenye ubora na zilizo na bei ya chini.
''Wateja wanatafuta bidhaa za simu zilizo bora duniani,tunaamini kwamba Zuri itaturuhusu kupata mauzo mazuri nchini Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla'',alisema Jamal.
Simu mpya aina ya Smartphone zaingia Dar es Salaam
Reviewed by Ino
on
10:55:00 AM
Rating:
No comments:
Post a Comment